• Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Ofisi |
    • Malalamiko |
Simanjiro District Council
Simanjiro District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Chimbuko/Asili
      • Ukubwa wa Eneo
      • People of Simanjiro
      • Hali ya Hewa
      • Economic Activities
      • Orodha ya Viongozi
    • Dira na Moto
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Organization Structure
    • Vitengo
      • Internal Audit
      • Law
      • Procurement and supply
      • Bees
      • Election
      • ICT
    • Idara
      • Administration and Management
      • Agriculture and Irrigation
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Primary Education
      • Secondary Education
      • Health
      • Land,Natural Resources and Environment
      • Community Development
      • Finance and Trade
      • Works and
      • Envirnment and Cleanliness
      • Water
    • Departiment/Units Activities
    • Linki ya Machapisho
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mineral Extraction
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Huduma za Halmashauri
      • Mipango na Mazingira
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
      • Vikao vya Waheshiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • By Laws
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
    • Report
  • Kituo cha Habari
    • Notice to the Public
    • National and Office gallery
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Makataba ya Picha

Chimbuko /Asili

1.0 UTANGULIZI

1.1 SURA YA WILAYA

Wilaya ya Simanjiro ni kati ya Wilaya tano (5) zinazounda Mkoa wa Manyara. Wilaya ilianzishwa mwaka 1993 ikimegwa kutoka wilaya ya Kiteto. Wilaya inapakana na wilaya ya Monduli upande wa Kaskazini Magharibi, wilaya za Arumeru, Hai na Moshi upande wa kaskazini, Kiteto upande wa kusini, Kondoa na Babati upande wa Magharibi na Mwanga, Same, Kilindi na Korogwe upande wa Mashariki. Wilaya ina eneo lenye jumla ya kilometa za mraba 20,591

 

1.2 JIOGRAFIA NA HALI YA HEWA YA WILAYA

Wilaya iko katika eneo la nyanda kame na mbuga, hivyo hupata mvua za wastani wa kati ya milimita 400 na 500 kwa mwaka. Wilaya ina vipindi viwili vya mvua ambavyo ni vuli na masika.  Mvua za vuli hunyesha kuanzia mwezi Novemba hadi Desemba na masika hunyesha kuanzia mwezi Machi hadi Mei.

1.3 UTAWALA  NA  IDADI YA WATU 

Wilaya ya Simanjiro ina Tarafa sita (6), Kata kumi na nane (18), Vijiji hamsini na saba (57) na Vitongoji mia mbili themanini na moja (281). Kwa mujibu wa matokeo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, Wilaya ilikuwa na jumla ya wakazi 178,693, kati yao Wanawake ni 89,718 na Wanaume 88,975.Kwa mwaka 2018 Wilaya inakadiriwa kuwa na jumla ya wakazi 219,131, kati yao wanawake 111,757 na wanaume 107,374 sawa na ongezeko la asilimia 3.2 kwa mwaka.

 

1.4  HALI YA ULINZI NA USALAMA WILAYANI

Hali ya ulinzi na usalama katika Wilaya ya Simanjiro ni ya kuridhisha kwani hakuna matukio makubwa ya kutisha isipokuwa uhalifu mdogo mdogo unaodhibitiwa na vyombo vya ulinzi na usalama. Mahusiano ya vyombo vya ulinzi na usalama,taasisi za serikali, vyombo vya utawala na uwakilishi wa wananchi,taasisi za kidini, mashirika ya umma na binafsi ni ya kuridhisha.Serikali ya wilaya imeendelea kusimamia mamlaka za Vijiji, Kata na Tarafa kutimiza majukumu yake kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni.

Kunapokuwepo na viashiria vya migogoro hushughulikiwa mapema na mamlaka ya Wilaya na kupatiwa ufumbuzi stahiki. Wilaya haina migogoro ya kidini, kisiasa wala ukabila.  

 

1.5 HALI YA SIASA NA UTAWALA NA JINSI MALALAMIKO /KERO MBALIMBALI ZINAVYOSHUGHULIKIWA 

Hali ya kisiasa ipo salama katika eneo lote la Wilaya na hakuna tukio lolote baya lililoripotiwa. Aidha vyama mbalimbali vya siasa vinafanya shughuli zake kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu. Kwa upande wa Malalamiko na kero, Wilaya ina utaratibu wa kutatua kero na malalamiko kwa njia mbalimbali zikiwemo mikutano ya hadhara, vikao mbalimbali katika ngazi za vijiji, kata mpaka Wilaya. Pia Wilaya imeanzisha madawati ya malalamiko katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji ambayo hushughulikia kero na malalamiko kutoka kwa jamii. Katika kipindi cha Januari hadi Aprili 2018 jumla ya kero 110 za watu binafsi zimepokelewa na kutafutiwa ufumbuzi kupitia madawati haya na migogoro ya mipaka 9 ilifanyiwa kazi na migogoro 2 inayohusisha ugomvi wa kijamii ilitatuliwa pia.

Matangazo

  • No records found
  • Ona vyote

Habari Mpya

  • Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro yaadhimisha siku ya Mapinduzi 12.1.2021 kwa upandaji wa miti

    January 12, 2021
  • UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAJI WILAYANI SIMANJIRO

    November 11, 2020
  • Ona vyote

Video

BILIONEA LAIZER AKABIDHI SHULE ALIYOIJENGA KWA SERIKALI
video Zaidi

Fika kwa Haraka

  • Matokeo kidato cha nne 2020/2021
  • Matokeao darasa la nne 2020/2021
  • Matokeo kidato cha pili 2020/2021
  • Mission and Vision
  • Organization Structure
  • Completed Projects

Kiungo Muunganisho

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Idara ya Habari-Maelezo
  • Tovuti kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Simanjiro Bomani street-Orkesumet

    Sanduku la Posta: P.o Box 9596,Orkesumet,Simanjiro,Manyara,Tanzania

    Simu: Tel:027-29707889

    Simu: +255-758350936

    Barua pepe: ded@simanjirodc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za siri
    • Kanusho
    • Website Map

copyright@2016 Halmashauri ya Wilaya Simanjiro.Haki zote zimehifadhiwa